Tibazetu Afrika

Blog hii inahusu tiba za asili juu ya magonjwa mbalimbali ya kimwili na kiroho.Habari,burudani na mambo yote yanayoizunguka jamii.

Contact us

+255 657 739713
Whatsapp/call and sms

Email
Tibazetutz@gmail.com

Watembeleaji

Search

Alhamisi, 1 Agosti 2019

Hii ni kwa wanandoa tu

Unarudi nyumbani jioni unamkuta mke wako hajaijipamba, Anajua umuhimu wa kujipamba kwa ajili ya mumewe  na ndivyo alivyo fundwa lakini hataki kuna kitu anaogopa endapo atajipamba.

Munapanda kitandani ukimgusa kama umegusa jiwe vile hana habari kabisa na anakwambia,  "Hebu niache bwana tulale kwanza,  mwenzio nina usingizi tena nimechoka mpaka baadae".

Munalala,  unamwamsha usiku wa manane anakufokea, "Mambo gani ya kuamshana usiku wa manane kwani hii daku?. Subiri mpaka alfajiri tutakapo amka kuswali kabisa".

Muadhini Swala swala anakuamsha,  "Mume  wangu muadhini huyo nenda Msikitini" kumbe anakufukuza kinamna"

Unarudi msikitini ile kugusa kitasa cha barazani mkeo anatoka chumbani na kwenda uani anaanza kufagia au kufua nguo.

Unaingia chumbani hukuti mtu unaanza kununa na unaogopa kumuita maana huo ukali utakao tolewa mwenyewe unaujua.

Unatulia kidogo unawaza la kufanya lakini huna, unaamuaa kuvaa na kuelekea kibaruani isije ukachelewa  ukapoteza kibarua,  siku imepita hiyo.

Kama majanga haya yapo nyumbani kwako basi ndoa imepigwa Husda kuna Jini mahaba anaivuruga.

Nini kifanyike?  Mpe maji ya Mkunazi yaliyo somewa Ruqya anywe na kuoga,  lnshaallah mitihani itaondoka.

Makala ijayo tutawazungumzia  wanaume walio athiriwa na Husda. katika ndoa zao.