Tibazetu Afrika

Blog hii inahusu tiba za asili juu ya magonjwa mbalimbali ya kimwili na kiroho.Habari,burudani na mambo yote yanayoizunguka jamii.

Contact us

+255 657 739713
Whatsapp/call and sms

Email
Tibazetutz@gmail.com

Watembeleaji

Search

Jumamosi, 12 Agosti 2017

mifupa ya paka mweusi aliyekufa husaidia kumuona mchawi au mwizi anayekuja usiku ukiwa umelala

Ukitaka kumuona mchawi/mwizi akija kwako usiku wakati upo usingizini utachukua mifupa ya paka mweusi aliyekufa au kuuliwa bila wewe kujua kauliwa na nani

Kisha utaiweka katika pembe nne za nyumba au milangoni na madirishani basi akija mchawi au mwizi wakati ukiwa usingizini utamuona bila yeye kujua kuwa anaonekana na utamtambua

Pia wachawi humtumia sana paka wanapotaka kutuma jini kwa mtu
Jini akitumwa kwa mtu hutumiwa zaidi paka au panya,myama au mdudu huyo huchunwa au hutolewa manyoya mkiani na kuchorwa majina ya iblis mkiani mwake kisha hutumwa kwa mtu fulani akamuingie,basi utajikuta unaumwa umwa tu bila kupona ukipima huonekani ugonjwa wa aina yoyote na ndoto zako nyingi zitakuwa ni kuota kushindwa kufanya jambo.mfano kama vile( kuota kuachwa na gari, kufeli mtihani,kurushiwa kitu na kushindwa kudaka) kuota sana upo darasani au shuleni na mpo mitihanin ila mwisho wa ndoto unaota wewe umefeli,ndoto hizi sio nzuri.

Mifupa yake wachawi huitumia kama kinga wakienda kuchawia huweka mifupa ya paka mdomoni basi akienda kuchawia popote hawezi kuonekana wala kudhurika kirahisi labda akutane na nguvu inayofanana nae au zaidi.

Jihadharini sana na ndoto za paka sio nzuri pia mara nyingi ukimuota paka huashiria ni mchawi huyo .