Tibazetu Afrika

Blog hii inahusu tiba za asili juu ya magonjwa mbalimbali ya kimwili na kiroho.Habari,burudani na mambo yote yanayoizunguka jamii.

Contact us

+255 657 739713
Whatsapp/call and sms

Email
Tibazetutz@gmail.com

Watembeleaji

Search

Jumatano, 23 Desemba 2015

TAFSIRI NDOTO ZAKO MWENYEWE[SEHEMU YA KWANZA]


MWANAMKE UKIOTA UNA NDEVU
Mwanamke ukiota una ndevu ni dalili ya kuwa hutazaa milele,na baadhi ya wafasiri wamesema ni dalili ya maradhi ambayo yatampata siku za usoni,au ziada ya mali ya mumewe na utukufu wa mwanawe wa kiume.


KAMA AKIWA AMEOLEWA
Ni ishara ya mumewe kuondoka


AKIWA NI MJAMZITO
Atazaa mtoto wa kiume na litatimia jambo lake


AKIOTA NDEVU ZIMEREFUKA NA KUWA NYINGI
Umri wake utakuwa mrefu na mali yake itazidi kuongezeka 


UKIOTA UNA MASKIO MATATU
Ni ishara ya kuwa na mke mmoja na mabinti wawili


UKIOTA UNA SIKIO NUSU
Inajulisha kifo cha mkeo na kuwa utaoa mwingine badala yake 


UKIOTA UNA MASKIO MANNE
Inajulisha moja kati ya mambo mawili
1.utakuwa na wake wanne 
2.mabinti wanne wasiokuwa na mama 


UKIOTA MASKIO YAKO YAMEJAZWA VITU NDANI YAKE
Ni dalili ya kuwa utakufuru


KUOTA MENO YANAVUNJIKA
Ni dalili ya kuwa utalipa deni lako kidogokidogo


UKIOTA MENO YANADONDOKA NA UNAHISI MAUMIVU 
Ni dalili ya kuondokewa na kitu katika vitu vilivyomo ndani mwako


UKIOTA MENO YAKO YA MBELE TUU YANADONDOKA
Ni dalili ya kuwa unazuiwa kufanya jambo lako ulilokuwa ukilifanya ima kwa vitendo au maneno


UKIOTA KITU KINATOKA MDOMONI MWAKO 
Ni dalili ya rizki utakayoipata iwe ni halali au haramu


UKIOTA UNA ULIMI MREFU
Ni dalili ya kushinda katika ufasaha wa kuongea  na adabu yako,upole na utukufu 



UKIOTA ULIMI WAKO UMEFUNGWA
Ni dalili ya ufukara na maradhi



UKIOTA UNA MENO MEUPE NA MAZURI
Ni dalili ya ziada katika nguvu na mali ya daraja ya juu kwa watu wa nyumbani mwake


UKIOTA UNA MENO YA DHAHABU
ukiwa ni mwenye elimu basi ndoto yako ina sifa nzuri,na ikiwa sio mwenye elimu basi basi ni dalili ya shari na watu wako watapatwa na maradhi au kuangamia


UKIOTA UNA MENO YA FEDHA
Ni dalili ya kupata hasara katika mali yako,na yakiwa ni meno ya kioo ni dalili ya umauti


KUOTA UNALISHA MASKINI
Utatoka kwenye majonzi na utapata amani kama ulikuwa na hofu


UKIOTA UNASWALI KATIKA ALKAABA
Utapata baadhi ya watukufu na viongozi na utapata amani na kheri


UKIOTA UMEKUFA NA KUFUFUKA
Utafanya madhambi na utamuomba mungu msamaha


 KUOTA UNAKUFA BILA KUUMWA
Umri wako utakuwa mrefuu


UKIOTA UMEKUFA,WATU WANAOMBELEZA NA KUKUFANYIA SHUGHLI ZA MAZISHI
Dunia yako itakuwa nzuri lakini akhera yako imeharibika


KUOTA MAITI INAJIOSHA YENYEWE
Watu wako watatoka kwenye majonzi na mali yao itazidi


KUOTA UNAONA SANDA
NI DALILI YA ZINAA


 UKIOTA SANDA IMEVESHWA LAKINI HAIJAKAMILIKA UVAAJI WAKE
Utatiwa kwenye zinaa lakini hutokubali


UKIOTA UMEFUNGWA KWENYE SANDA VILEVILE KAMA MAITI
Ni ishara ya kifo chako


KUOTA UPO KWENYE JENEZA
Utajenga udugu na mtu kwa ajili ya mungu


UKIOTA UPO KWENYE JENEZA NA WATU WAMELIBEBA 
Utatawala na kupanda daraja na watu watakufuata kama ulivyowaona ndotoni


UKIOTA UMEBEBA MAITI
Utapata mali ya haramu


UKIOTA UNAMPELEKA MAITI SOKONI
Utapata mahitaji yako na faida kwenye biashara zako

UKIOTA JENEZA LINAPITA HEWANI
Atakufa mtu mkubwa kama rais,mwanachuoni au yeyote mwenye daraja ya juu

UKIOTA UMEKUFA NA UNAZIKWA 
Utasafiri safari ya mbali na utapata mali 

KUOTA UMEMFUFUA MAITI
Utamsilimisha mtu wa dini nyingine kuwa muislam au mtu muovu atatubia dhambi zake kwako


UKIMUOTA DADA YAKO ALIYEKUFA ANAISHI
Utajiwa na mgeni kutoka safarini na utafurahi

UNGANA NAMI KATIKA SEHEMU YA PILI