Tibazetu Afrika

Blog hii inahusu tiba za asili juu ya magonjwa mbalimbali ya kimwili na kiroho.Habari,burudani na mambo yote yanayoizunguka jamii.

Contact us

+255 657 739713
Whatsapp/call and sms

Email
Tibazetutz@gmail.com

Watembeleaji

Search

Jumatatu, 14 Desemba 2015

TIBA YA MTU ANAYEKOJOA KITANDANI


Daktari Zaki Almallah , mtaalam wa vibofu vya mikojo anasema tabia ya watu wazima kuwa vikojozi inarithishwa, kama baba au babu alikuwa kikojozi basi kuna uwezekano wa asilimia 40 kwa mtoto au mjukuu kuwa kikojozi ukubwani.

Wataalam katika Hospitali ya Birmingham nchini Uingereza wanasema sababu nyengine ni kutokomaa kwa tezi ya pituitary gland inayopatikana ndani ya ubongo chini ya sikio.

tezi hii hutoa homoni yake na chembechembe zake wakati wa usiku hivyo kuzuia utengenezaji wa mikojo. hivyo tezi hiyo ya pituitary gland ikiwa dhaifu au haikukomaa basi chembechembe hizo zitatuma ujumbe kuwa mikojo zaidi itengenezwe, hivyo basi mtu kuwa na balaa ya kujikojolea akiwa amelala maana ni lazima zitoke.
Mtu kuwa na stress,au msongo kuna weza kumsababishia mtu huyo matatizo ya ukojozi.

ILI KUJITIBU TATIZO HILI
Zipatikane kwato za mbuzi na mgonjwa aziunguze moto na azisage vizuri apate unga,
baada ya hapo changanya unga huo na asali safi ya nyuki kwa uwiano ulio sawa
asubuhi kabla hajala chochote ale kijiko1cha chakula,mchana na jioni pia akienda kulala.
 afanye hivi kwa siku 11 atapona na kama ni mtoto basi atumie kijiko cha chai