Tibazetu Afrika

Blog hii inahusu tiba za asili juu ya magonjwa mbalimbali ya kimwili na kiroho.Habari,burudani na mambo yote yanayoizunguka jamii.

Contact us

+255 657 739713
Whatsapp/call and sms

Email
Tibazetutz@gmail.com

Watembeleaji

Search

Jumanne, 25 Oktoba 2016

UJUE UCHAWI WA MAFUSHO NA MAFUSHO YA KILA NYOTA


PUNDA (QIST)
Mafusho haya yako kama vijiti, yana rangi ya kahawia ni kwa wenye nyota ya Punda, siku yao ni Jumanne, unachoma kati ya saa 12-1 asubuhi na saa 7-8 mchana.

NG’OMBE (MUSTAKA)
Mafusho haya yako kama vijiwe vidogo vidogo vyenye vumbi na vina rangi ya kijivu jivu na ni kwa wenye nyota ya Ng’ombe, siku yao ni Ijumaa unachoma kati ya saa 12-1 asubuhi na saa 7-8 mchana.

MAPACHA (KACHIRI)
Mafusho haya yako kama mauwa yaliyo kauka na rangi yake ni kahawia na ni ya wenye nyota za Mapacha, siku yao ni Jumatano choma kati ya saa 12-1 asubuhi au kati ya saa7-8 mchana.

KAA (UBANI)
Hapa unaweza kutumia ubani wa aina yeyote wakawaida au ubani maka unachoma siku ya Jumatatu kati ya saa 12-1 asubuhi na saa7-8 mchana. Nyota yake ni Kaa (CANCER)

(SIMBA) (SANDARUS)
Mafusho haya yako kama mawe yenye rangi ya njano ni kwa wenye nyota ya Simba (Leo) ambao siku yao ni Jumapili, unachoma katika muda wa Shams ambao ni kati ya saa12 asubuhi na saa moja asubuhi au saa saba mpaka saa nane mchana

MASHUKE (KACHIRI)
Mafusho haya yako kama mauwa yaliyo kauka na rangi yake ni kahawia na ni ya wenye nyota ya mashuke, siku yao ni Jumatano choma kati ya saa 12-1 asubuhi au kati ya saa7-8 mchana

MIZANI MUSTAKA
Mafusho haya yako kama vijiwe vidogo vidogo vyenye vumbi na vina rangi ya kijivu jivu na ni kwa wenye nyota ya Mizani, siku yao ni Ijumaa unachoma kati ya saa 12-1 asubuhi na saa 7-8 mchana.

NGE(QIST)
Mafusho haya yako kama vijiti, yana rangi ya kahawia ni kwa wenye nyota ya Nge, siku yao ni Jumanne, unachoma kati ya saa 12-1 asubuhi na saa 7-8 mchana.

MSHALE- UDI-KAFURU
Hapa unaweza kutumia udi wa aina yeyote ambao unachanganya na kafur. Hii kafur ina rangi nyeupe na mafusho haya ni kwa wenye nyota ya Mashale, siku yao ni Alhamisi unachoma kati ya saa 12-1 asubuhi au saa 7-8 mchana.

MBUZI MIATUN – SAILA
Mafusho haya yako kama lami nyeusi, yana mafuta mafuta na yana harufu kama mvuje ni kwa wenye nyota ya Mbuzi, siku yao ni Jumamosi unachoma kati ya saa 12-1 asubuhi na saa 7-8 mchana


NDOO MIATUN – SAILA
Mafusho haya yako kama lami nyeusi, yana mafuta mafuta na yana harufu kama mvuje ni kwa wenye nyota ya Ndoo. siku yao ni Jumamosi unachoma kati ya saa 12-1 asubuhi na saa 7-8 mchana.


SAMAKI UDI-KAFURU
Hapa unaweza kutumia udi wa aina yeyote ambao unachanganya na kafur. Hii kafur ina rangi nyeupe na mafusho haya ni kwa wenye nyota ya Samaki, siku yao ni Alhamisi unachoma kati ya saa 12-1 asubuhi au saa 7-8 mchana.


UCHAWI WA MAFUSHO
Unaweza ukatumia mafusho katika kufanya watu wapendane au watengane. Kupendana kwa maana mapenzi yaendelee kuwepo au ndoa ishamiri na kutengana kwa maana ya kuvunja ndoa au kufarakanisha walo pamoja


MAPENZI

Ukitaka watu wapendane unatumia mafusho yafuatayo:
Ambar na udi, Rawandi, Kafur, Zafarani na Mustaka. Mchanganyiko huu unachoma katika siku za Alhamis au Ijumaa au Jumatatu kwa kutia nia ya jambo la mapenzi ulitakalo au unaweza kuchoma siku yoyote katika saa za Atlarid, Zuhura au Qamar.

KUGOMBANISHA
Ukitaka kugombanisha unatumia mafusho yafuatayo:
Sandal nyekundu, Halititi,washqu (watu) na Miatun saila
Unachoma mafusho hayo siku ya Jumamosi au Jumanne au siku yeyote katika saa za Zohal au Mariikh kwa kutia nia ya kutaka hao unaowataka wagombane au kufarakana.

ONYO
usigombanishe watu bila sababu yenye mashiko itakurudia