Tibazetu Afrika

Blog hii inahusu tiba za asili juu ya magonjwa mbalimbali ya kimwili na kiroho.Habari,burudani na mambo yote yanayoizunguka jamii.

Contact us

+255 657 739713
Whatsapp/call and sms

Email
Tibazetutz@gmail.com

Watembeleaji

Search

Jumapili, 18 Machi 2018

Mzimu ni nini?


Zipo nadharia nyingi zinazo elezea mzimu ni kitu gani, nadharia iliyo zoeleka ni ile inayosema mzimu ni roho ya mtu aliye kwisha kufa. Mtu huyo anaweza kuwa amekufa zamani sana, ama muda mfupi ulio pita.
Mzimu ni nishati ( energy), roho au haiba ( personality) ya mtu ambaye amefariki dunia lakini imekwama katika sehemu iliyo kati ya duniani ( ulimwengu wa nyama/ulimwengu unao onekana ) na mahali ambapo roho hiyo inatakiwa kwenda kuishi baada ya maisha ya hapa duniani kukamilika ( ulimwengu usio onekana/ afterlife/ land of the souls )
. Watafiti wengi wana amini kuwa roho hizi zinakuwa hazijui kama zimekufa katika ulimwengu wa nyama ama hazitaki kuamini kama zimekufa katika ulimwengu wa nyama ama hazikubaliani na kifo chao katika ulimwengu wa nyama. Mara nyingi roho hizi huwa ni roho za watu ambao walikufa katika mazingira yanayo tatanisha kama vile kufa kwa kuuliwa bila sababu ( cold blood), kutolewa kafara, ama kufa baada ya maisha ya msukuleni. Kwa ufupi hizi huwa ni roho za watu ambao walidhulumiwa haki yao ya kuishi hapa duniani. Mizimu inaweza kujidhirisha na kuonwa na wanadamu ama wanyama katika namna tofauti tofauti kama vile muonekano ( hapa mizimu ,huwatokea ndugu, jamaa na marafiki zao wakiwa katika maumbo ya sura zao wakati wanaishi duniani na mara nyingi huwatokea wakiwa na nguo walizo penda kuzivaa wakati wa uhai wao ), sauti, harufu( hapa kwenye harufu mzimu unapo mtokea muhusika,hujidhihirisha kwa harufu yake ya mwili ( kila mtu ana harufu yake ya mwili, watu huweza kuwatambua watu wao wa karibu kwa harufu zao za mwili ), ama pafyumu ( katika pafyumu, mzimu utamtokea mtu kwa harufu ya marashi ambayo alikuwa anapenda kuyatumia wakati yupo duniani katika ulimwengu wa nyama. Wakati mwingine, mzimu huweza kuwatokea ndugu jamaa na marafiki zake kwa kuwashika.
Kwa ufupi mzimu huwa ni roho ambayo imewahi kuishi katika ulimwengu wa nyama kama mwanadamu ama mnyama.