Tibazetu Afrika

Blog hii inahusu tiba za asili juu ya magonjwa mbalimbali ya kimwili na kiroho.Habari,burudani na mambo yote yanayoizunguka jamii.

Contact us

+255 657 739713
Whatsapp/call and sms

Email
Tibazetutz@gmail.com

Watembeleaji

Search

Alhamisi, 28 Januari 2016

VITU VINAVYOONGEZA MAZIWA KWA MAMA ANAYENYONYESHA


~Kuna baadhi ya akina mama wanapotoka kujifungua 
katika kipindi kile muhimu cha kunyonyesha huwa 
maziwa yanakuwa kidogo sana kiasi cha kutomtosheleza
 mtoto


~tatizo hili ni baya kwa sababu mtoto anapozaliwa 
anahitaji sana kupata maziwa ya mama ya kutosha kwa
 muda usiopungua miezi 6


~maziwa ya mama yana lishe zote zinazohitajika kwa 
mtoto na kama mtoto huyu atapata maziwa ya kutosha
 basi bila shaka atakuwa ni mwenye afya njema na 
watoto wanaopata maziwa kidogo afya zao huwa si 
njema sana.


JINSI YA KUONDOA TATIZO HILI

~Kuna njia nyingi za asili katika kuondoa hili tatizo,lakini
 kwa leo ntazungumzia njia chache tuu ambazo ni 
muhimu zaidi na ndizo zinazojaza haraka maziwa kifuani 
kwa mama mwenye mtoto mchanga


SUPU YA NG'OMBE,MBUZI NA KONDOO

~Mwanamama anapotoka kujifungua ni vizuri apate supu
 kila asubuhi na ni vizuri zaidi akapata supu ya 
kongoro,nyama ya ngombe au supu ya kondoo kwani 
supu za namna hii ni tiba nzuri kwa mama mwenye 
matatizo ya kutopata maziwa ya kutosha kwa ajili ya 
mtoto wake na pia hurejesha nguvu zilizopotea wakati
 wa mshikemshike wa kujifungua.


                          NDIZI ZA KUCHEMSHA

~Pia ndizi za kuchemsha ni nzuri sana kwa kuondoa hili 
tatizo la kukosa maziwa kwa mama 
mjamzito,zichemshwe vya kutosha mpaka ziwe laini na
 hata mtori pia unafaa katika kutibu hali hyo


                                     MAJI

~Mzazi anapaswa awe ni mwenye kujitahidi kunywa maji
 ya kutosha kila siku kwani nayo humsaidia kuongeza 
maziwa kwa ajili ya mwanae mpya,pia mzazi kukandwa
 maji ya moto sehemu za siri si chini ya wiki moja ni
 vizuri zaidi kwani humsaidia kupata nguvu na kuufanya 
uke hurudi katika hali ya kawaida kwa muda mfupi.


UJI WA PILIPILI MTAMA

~Aidha mzazi anashauriuwa anywe uji wenye pilipili 
mtama na sio pilipili hizi za chachandu,kwani pilipili
 mtama zina faida mbili kwa mzazi

1.huondoa haraka makovu yaliyotokana na msuguano
 wa mtoto tumboni

2.husaidia ongezeko la maziwa ya mama ili yapatikane 
ya kutosha kuweza kumnyonyesha mwanae na akapata
 afya njema



KWA TIBA NA USHAURI WASILIANA NASI
                              KWA
 
                           0653 532036

               AU TUANDIKIE BARUA PEPE

                 TIBAZETUTZ@GMAIL.COM