Tibazetu Afrika

Blog hii inahusu tiba za asili juu ya magonjwa mbalimbali ya kimwili na kiroho.Habari,burudani na mambo yote yanayoizunguka jamii.

Contact us

+255 657 739713
Whatsapp/call and sms

Email
Tibazetutz@gmail.com

Watembeleaji

Search

Jumamosi, 30 Aprili 2016

JE UNAIJUA NAFASI YAKO YA KUPATA PESA?

PESA NI NINI????????????????????????????
Pesa inatambulika kama nyenzo ya kukuwezwesha kupata
 kitu au huduma, lakini kwa watu wengine huchukuliwa
 katika tafsiri tofauti,Kwa wengine pesa kwao huwa ni
 ulinzi na furaha na kwa wengine huwa ni starehe au njia
 ya kumaliza matatizo aliyonayo huyo muhusika.

Lakini kuna upande mwingine wa Pesa, namna gani
 unaweza kuipata au kuivuta ije kwako.

Hujawahi kusikia watu wakisema hata wewe ukisema
kwanini Fulani anatengeneza pesa kuliko mimi na
 inawezekana wewe na yeye mumezaliwa tarehe moja na
 nyota yenu ni moja.

Pamoja na kwamba nyota yako inachangia katika wewe
 kupata pesa kuna mambo mengine yanaweza kukupa
 mchango mkubwa katika kupata pesa mfano,sehemu
 ulipozaliwa, elimu yako, makuzi ya wazazi wako, pamoja
 na mambo mengine ni moja wapo ya mambo ambayo
 yanachangia wewe kuwa na Uchumi mzuri au kivutio cha
 Pesa.


Wakati mwingine sio wewe hata mimi huwa najiuliza ni
 kwa nini watu wanaozaliwa tarehe mmoja mwezi mmoja
 lakini huwa wanatofautiana mwingine tajiri na mwingine
 maskini au hana kitu!!!!!.

Kwanza kabisa Jina lako ni muhimu sana, kama ilivyo
 tarehe yako ya kuzaliwa katika kukusaidia wewe kupata
Mfano unampa mtoto jina Matatizo,shida au tabu
na kadhalika.

Jina huwa linaweza kubadilishwa lakini tarehe ya
 kuzaliwa haibadiliki kama ilivyo Mshale wa Kampasi
ambao saa zote huwa unaelekea kaskazini………


Hii ndio sababu kila tarehe lazima iwe na maelezo yake
 ya namna ya kufanya ili kuweza kupata mafanikio

Mfano Hata ukiwa umezaliwa tarehe moja na mtu
 mwingine hamuezi kuugua ugonjwa mmoja au kuoa
 tarehe moja na wala kuweza kupata mafanikio wakati
 mmoja, kwa hiyo tofauti zilizopo za namna ya kupata
 pesa ni lazima zieleweke.


UNAIJUA NAFASI YAKO YA KUPATA PESA?
Ikiwa umezaliwa tarehe 1 10, 19, 28 ya mwezi wowote Au
 kama hujui tarehe yako ya kuzaliwa ikiwa jina lako
 limeanzia na Herufi za (A, J, S.) wewe huwa 
unazichukulia pesa kama njia ya kumaliza matatizo yako 
au njia ya kuinua jina lako, hadhi yako au nafasi yako 
kimaisha na katika Jamii.

Njia nzuri ya wewe kupata pesa ni kujiingiza katika
 Nyanja au kazi ambazo ni mpya na halisi au za uhakika
 , kwa maana ya kufanya Biashara mpya kuwa na miradi 
mingi kwa wakati mmoja au huku unafanya kazi huku 
unafanya biashara.

Kama ilivyo tarehe yako ya kuzaliwa unatakiwa uwe na
 mamlaka juu ya wengine kwa maana ya kwamba uwe
 wewe ndie mmiliki wa shughuli, kama kampuni yako
 mwenyewe na siyo kuajiriwa au kutumwa

Jitegemee, jitume na uwe ni wewe, jaribu kuwa na hisia 
au mawazo ya kufanikiwa na mara kwa mara buni njia 
tofauti za kupata pesa tena nyingi.Jaribu kuwa
 muaminifu na kopa katika Taasisi zinazoeleweka. Miezi
 ya Februari, April na Agosti ndio miezi yako ya
 mafanikio,katika utekelezaji wa Shughuli zako jaribu
 sana kuwa makini na mfuatiliaji wa mambo yako 
usiwaachie watu. Tahadhari katika miezi ya Januari, May 
na Oktoba, hii siyo miezi mizuri kwako usikope wala 
kukopesha au kuanzisha shughuli yoyote ya kipato 
katika miezi hiyo.

Waliofanikiwa katika kipengele hiki ni kama hawa
wafuatao:-

1. Dolly Patron alizaliwa tarehe 19/1/1964

2. Rod Stewart alizaliwa tarehe 10/1/1945

3. Lee Marvin alizaliwa tarehe 19/2/1964

4. Jacqueline Kennedy onasis alizaliwa tarehe 28/2/1926

5. Lisa marie Presley alizaliwa tarehe 1/2/1929

6. Bruce willis alizaliwa tarehe 19/3/1955

7. Evander holyfield alizaliwa tarehe 19/10/1962

8. William Bill Gate alizaliwa tarehe 28/10/1
955

9. Ted Turner alizaliwa tarehe 19/11/1938.


WATU WA NAMBA MBILI

Ikiwa umezaliwa tarehe 2 11, 20, 29 ya mwezi wowote
Au kama hujui tarehe yako ya kuzaliwa ikiwa jina lako
limeanzia na Herufi za (B, K, T.) Wewe huwa unakuwa
na aibu katika utafutaji wa Pesa hasa katika shughuli 
zako mwenyewe.

Njia nzuri sana kwako wewe kupata pesa ni kwa
kuzikusanya na kuzihifadhi kidogo kidogo kwa muda
mrefu, kwako wewe kinyota huwezi kupata pesa nyingi
kwa wakati mmoja na huwa
zinakuja ukiwa unajishughulisha na shughuli
 zinazohusiana na jamii, mambo ya ubunifu, mbinu na
mipango ya watu ambao mnaelewana au wako tayari
kushirikiana na wewe, hiyo itakuongezea spidi ya wewe 
kupata pesa.

Jiunge katika kusaidia watu hiyo itakuletea faida ya
 kifedha baadae, Biashara ya kununua na kuuza itakupa
 faida kubwa. Shughuli zako za kipato kubwa zifanyike
 kwa ushirikianao na watu waliozaliwa Mwezi January, May, July na Oktober

Kuwa na tahadhari kukopa pesa au kujiingiza katika
biashara miezi ya April, November na Januari.

Waliofanikiwa ambao ni Mamilionea katika kipengele hiki 
ni kama hawa wafuatao:-
1. Oprah Winfrey alizaliwa tarehe 20/1/1954

2. Michael Jackson alizaliwa tarehe 29/8/1958

3. Spike lee alizaliwa tarehe 20/3/1957

4. Cindy Crawford alizaliwa tarehe 20/2/1966

5. Andre Agassi alizaliwa tarehe
29/4/1970


WATU WA NAMBA TATU
Ikiwa umezaliwa tarehe 3 12, 21, 30 ya mwezi wowote
 Au kama hujui tarehe yako ya kuzaliwa ikiwa jina lako
 limeanzia na Herufi za (C, L, U.)

Wewe ni mtu ambaye huwa unaishi kwa wakati huo uliopo, kwa maana unatumia unachokipata kila
 
kinapokuja, hali hii inakufanya utumie hata akiba yako
 uliyonayo au mtaji wako ulionao. Njia nzuri ya
 kukufanya uwe na pesa nyingi ni kujithibiti, Ukifikiri
 makubwa basi utafanikiwa pakubwa, neno kushindwa
 lisiwe lako, ukiwa na tabia ya kujiamni utafanikiwa sana.

Kopa, kuwa muaminifu na lipa madeni yako kwa wakati,

 muda mzuri wa wewe kupata pesa ni Mwezi wa March,
 May, Oktober na Decemba, miezi ambayo unaweza
kupata matatizo ya kifedha ni mwezi wa February, June
 Agosti na September

Waliofanikiwa ambao ni Mamilionea kwa kipengele hiki
 ni hawa wafuatao:-

1. Bill Cosby alizaliwa tarehe 12/7/1937

2. Mike Tyson alizaliwa tarehe 30/6/1966

3. Eddie Murphy alizaliwa tarehe 3/4/1961

4. Mel Gibson alizaliwa tarehe 3/1/1956

5. Tiger Woods alizaliwa tarehe 30/12/1975


WATU WA NAMBA NNE

Ikiwa umezaliwa tarehe 4 13, 22, 31 ya mwezi wowote
 Au kama hujui tarehe yako ya kuzaliwa ikiwa jina lako 
limeanzia na Herufi za (D, M, V.)

Wewe ni mmoja ya watu ambao unaweza au unapata pesa
 zako kwa wingi sana katika njia ambao si za kawaida.

 Kuna wakati unaweza ukawa na pesa nyingi sana na kuna
 wakati unakuwa huna kitu kabisa. Unaweza kuwa
 tofauti na pesa lakini una njia ya kuzitumia unapozipata

unatakiwa ili kuhifadhi hizo pesa uishi kwa kuwa na
 rekodi nzuri ya fedha, bajeti nzuri na matumizi yako
 yaendane na kipato chako, unapofanya manunuzi jaribu
 kulilia hali, nunua vitu vya bei ya chini na utapata
Maendeleo Makubwa katika pesa.


Biashara na masuala ya kipato yafanyike mwezi wa 
Februari, June, na Agosti , miezi mibaya kwako kifedha 
ni mwezi wa January, May na Oktoba.

Waliofanikiwa ambao ni Mamilionea kwa kipengele hiki ni 
hawa wafuatao:-

1. Stevie Wonder alizaliwa tarehe 13/5/1950

2. Clint Eastwood alizaliwa tarehe 31/5/1966

3. Wesley Snipes alizaliwa tarehe 31/7/1962

4. Naomi Campbell alizaliwa tarehe 22/5/1970

5. Dennis Rodman alizaliwa tarehe 13/5/1964


WATU WA NAMBA 5
Ikiwa umezaliwa tarehe 5 14, 23, ya mwezi wowote Au
 kama hujui tarehe yako ya kuzaliwa ikiwa jina lako
 limeanzia na Herufi za (E,N, W.)

Wewe ni mtu ambaye unapenda kuishi kwa wakati, (kwa
 maana ya kutumia kilichopo kulingana na hali yako), hali
 hii au tabia hii uliyonayo huathiri sana kipato chako.

Huna tabia nzuri ya kuhifadhi fedha. Wewe ni mtu 
ambaye unaweza kupata fedha kwa kufanya majaribio,
 bila ya kuwa na tahadhari (Usiwe muoga) na kwa
 kubahatisha.

Ukiwa na shughuli zaidi ya moja inaweza kukusaidia sana
 kupata pesa za ziada

Kwa vile number 5 ni namba ya Habari na Matangazo,
 jitangaze na sana jiuze kwa kutumia Radio, Televisheni,
 Magazeti utapata mafanikio makubwa.

Ukikumbuka kujilipa wewe kwanza kabla hujawalipa 
wengine utaona kwamba kipato chako kitakuwa sana na 
kwa haraka.

Mafanikio yako ya kipesa huwa yanapatikana Sana mwezi 
wa February, May na June na miezi mibaya kwako kipesa
 ni mwezi wa January, March na December

Waliofanikiwa ambao ni Mamilionea kwa kipengele hiki ni
 hawa wafuatao:-

1. Julio iglesias alizaliwa tarehe 23/9/1944

2. Michael Caine alizaliwa tarehe 14/3/1933

3. Prince Charles alizaliwa tarehe 14/11/1948

4. Quincy Jones alizaliwa tarehe 14/3/1933

5. Colline Powell alizaliwa tarehe 5/4/1937


WATU WA NAMBA 6

Ikiwa umezaliwa tarehe 6 15, 24, ya mwezi wowote Au 
kama hujui tarehe yako ya kuzaliwa ikiwa jina lako
 limeanzia na Herufi za (F,O, X.)

Njia nyepesi kabisa ya wewe kupata mafanikio ya kipesa
 ni kujituma kuwajibika kwa matendo yako, kwa maana
 mafanikio yanakuwa yako, kukosa kwako ni jambo la
 kawaida na mapingamizi kwako iwe ni changamoto ya
 kujituma zaidi na sio kukata tamaa.

Njia nyingine uliyonayo ya kupata pesa ni kuwa una hisia 
ya thamani unajua thamani ya pesa, unapokuwa unafanya
 biashara unakuwa asilia kwa maana biashara iko ndani ya
 damu yako, unaweza ukamuuzia mtu kitu hata kama 
hakitaki na unaweza kulilia hali pale inapotakiwa.

Kwa vile namba hii ni ya ushirika au ushirikiano
 utafanikiwa sana ukiwa utawashirikiasha wenzio katika
 mambo yako usifanye mambo peke yako

Hata hivyo fikra za kutokufanikiwa au kuwa na wasiwasi 
kwamba watu watakufikiriaje zinaweza kukuzuia usipate
 utajiri.

Fanya masuala ya kipesa mwezi wa Machi, May, July na
Oktoba. Jaribu sana kuepuka miezi ya Februari, Aprili na
Agosti

Waliofanikiwa ambao ni Mamilionea kwa kipengele hiki ni 
hawa wafuatao:-

1. Sylvester Stallone alizaliwa tarehe 23/9/1944


WATU WA NAMBA 7

Ikiwa umezaliwa tarehe 7 16, 25, ya mwezi wowote Au 
kama hujui tarehe yako ya kuzaliwa ikiwa jina lako 
limeanzia na Herufi za (D, M, V.)

Wewe ni mtu ambaye pesa zako hupatikana kwa pole 
pole na umakini mkubwa.ili kupata hayo mafanikio ya
 kipesa, Unatakiwa uwe una uelewa mkubwa katika
 utafutaji wa pesa, kwa maana kwamba uwe unajua 
unafanya nini au unataka kufanya shughuli gani katika 
kutafuta pesa. Jambo hilo litakusaidia sana katika kujua
 pesa utazipataje.

Katika utafiti wangu wa mamilionea sikushangaa sana
 kuona kwamba wale wote waliozaliwa katika namba 7 
wamekuwa ni watu wa nyuma nyuma au wenye aibu
 katika utafutaj pesa. Hasa ikizingatiwa kwamba namba 
saba ni namba ya kiroho na kimungu na siyo ya kidunia .

Ukitaka mafanikio ya kipesa ni lazima uwe na Ubunifu na
 utambuzi wa nini unataka, hali hiyo itakusaidia sana kwa
 uwezo wa juu kuvutia mambo yote yanayohusiana na
 wewe kupata pesa.

Yaweke pembeni na usiyaone 
kabisa yale ya kidunia 
ambayo yanaweza kukusababishia wewe kupoteza fedha 
hata zikiwa kidogo, Tumia mbinu zako na uelewa wako
 ambao umeupata kwa miaka mingi, ukiwa katika hali hii 
itakusaidia sana kuweke kupata mafanikio,

Kwa vile dunia ya sasa ni ya khabari na teknologia tumia
 uwezo wako katika hayo na utaona mafanikio makubwa

Muda mzuri wa wewe kufanya biashara ni miezi ya May,
 July, na Agosti na miezi mibaya ya kifedha ni Januari,
April na November.

Waliofanikiwa ambao ni Mamilionea wa kipengele hiki ni 

hawa 
wafuatao:-

1. Kareem Abduljabar alizaliwa tarehe 16/4/1947

2. Sean Connery alizaliwa tarehe 25/8/1930

3. Madonna alizaliwa tarehe 16/8/1958

4. Will Smith alizaliwa tarehe 25/9/1968

5. Elton John alizaliwa tarehe 25/3/1947

6. John F Kennedy Jr alizaliwa tarehe 25/11/1960

7. David Copperfield alizaliwa tarehe 16/9/ 1956

8. Nicholas Cage alizaliwa tareh
e 7/1/1964