Tibazetu Afrika

Blog hii inahusu tiba za asili juu ya magonjwa mbalimbali ya kimwili na kiroho.Habari,burudani na mambo yote yanayoizunguka jamii.

Contact us

+255 657 739713
Whatsapp/call and sms

Email
Tibazetutz@gmail.com

Watembeleaji

Search

Jumamosi, 30 Aprili 2016

YAJUE MAUMBO NA SURA ZA MAJINI KULINGANA NA SAYARI ZAO WANAZOTAWALA



MAJINI WA SATURN (ZOHALI) -MAJINI WA JUMAMOSI
Majini hawa huwa ni warefu, wembamba na wenye sura
ya ukatili na kutisha, wana nyuso nne ambazo kila moja
iko kila upande wa kichwa, yaani kwa mbele na nyuma
sura inakua na midomo kama ya ndege.

Pia wana sura nyeusi inayon’gaa katika kila goti. Mwendo
wao ni kama mwendo wa upepo ambao huambatana na 
radi.

Alama yao ni ardhi nyeupe kuliko theluji.

Umbo lao maalum ni kama Mfalme mwenye ndevu
anaemuendesha DRAGON.

Umbo lingine ni la mtu mzee mwenye ndevu

Umbo lingine ni la Bibi kizee ambae anaegemea kitu

Umbo lingine ni la Mvulana

Umbo lingine ni la Dragon

Umbo lingine ni la Bundi (Owl)

Umbo lingine ni la Nguo nyeusi isiyo na mwili

Umbo lingine ni la Ndoano au Mundu

Umbo lingine ni la mti wa Mreteni
Hawa ndiyo majini wanaotawala siku ya jumamosi


Majini wa Sayari ya Jua (Shams) - Majini wa Jumapili
Majini wa Sayari ya Jua (Shams) wana viungo na umbo la
 kati, wasiovutia na dhalimu, wana Sura nyekundu na 
rangi ya dhahabu iliyochanganyikana na Damu.

Mwendo wao ni mfano wa Umeme na Alama yao kubwa
 ni kusababisha mwenye kumuita kutokwa na jasho jingi

Umbo lao maalum ni la Mfalme aliyebeba fimbo ya
 kifalme huku akiwa amempanda Simba.

Umbo lao lingine ni la Mfalme aliyevikwa Taji.

Umbo lao lingine ni la Malkia mwenye Fimbo ya Kifalme.

Umbo lao lingine ni la Ndege wa aina yeyote isipokuwa
 wale ndege ambao wanawakilisha peponi.

Umbo lao lingine ni la Simba.

Umbo lao lingine ni la Jogoo.

Umbo lao lingine ni la Nguo ya Dhahabu isiyokuwa na mwili.

Umbo lao lingine ni la Fimbo ya Kifalme.

Umbo lao lingine la mwisho ambalo kwa kweli ni la
 kutisha sana; ni lile la Kiumbe ambaye haeleweki
 eleweki vizuri na ni vigumu kumuelezea ila ana mkia.
hawa  ndiyo majini wanaotawala siku ya jumapili


Majini wa Sayari ya Moon (Qamar) - Majini wa Jumatatu
Majini wa Sayari ya Moon – Mwezi (Qamar) wana Maumbo
makubwa, Laini, Tulivu na rangi yao ni kama wingu jeusi.
Muenekano wao ni umbo lililotuna, Vichwa vyao vina
upara, Macho yao ni Mekundu na yanatoa Majimaji, Meno
yao ni kama ya Nguruwe Mwitu.

Mwendo wao ni kama Dhoruba kubwa Baharini. Alama yao
ni ni Mvua kubwa inayonyesha katika Mduara.

Umbo lao Maalum ni Ni la Mtu kama Mfalme anayerusha
 Mishale huku akiwa anamuendesha Swala Jike.

Umbo lao lingine ni la Kijana Mdogo wa Kiume.

Umbo lao lingine ni la Mwindaji wa Kike mwenye Upinde
 na Mishale.

Umbo lao lingine ni la Ng’ombe.

Umbo lao lingine ni la Swala Mdogo.

Umbo lao lingine ni la Bata.

Umbo lao lingine ni la Nguo isiyokuwa na Mwili yenye
rangi ya Kijani au Fedha.

Umbo lao lingine ni la Mshale.

Umbo lao lingine ni la Kiumbe mwenye Miguu Mingi mfano
wa Tandu
hawa ndiyo majini wanaotawala siku ya jumatatu


 Majini wa Mars (Mariikh) - Majini wa Jumanne
Majini wa Mars (Miriikh) wanakuwa na Umbo refu, Mwili 
Mwekundu, mchafu na hutoa harufu yenye kutia kinyaa.
Huwa wanajitokeza pia katika mwili wenye rangi
Nyekundu, Kahawia au Nyeusi. Wana mapembe kama ya
mnyama aitwaye Ayala (Hart), kucha kama za
Simba,Wanatoa sauti kama za Nyati (Mbogo).

Mwendo wao ni kama mwendo wa moto unaowaka na
 Alama yao ni radi na umeme unaowaka kwa katikati.

Umbo lao maalum ni la Mfalme aliyevalia kivita akiwa
amempanda Mbweha (Mbwa mwitu).

Umbo lao lingine ni la Mwanamme aliye na silaha.

Umbo lao lingine ni la Mwanamke aliyeshikilia Ngao
kwenye mapaja yake.

Umbo lao lingine ni la Mbuzi Jike.

Umbo lao lingine ni la Farasi.

Umbo lao lingine ni la Paa.

Umbo lao lingine ni la Nguo Nyekundu isiyokuwa na
 mwili.

Umbo lao lingine ni la Sufi.
hawa ndiyo majini wanaotawala siku ya jumanne


 Majini wa Sayari ya Mercury (Attwarid) - Majini wa
 Jumatano
Majini wa Sayari ya Mercury (Attwarid) mara nyingi
 hutokea na mwili wa Kati, Baridi, Majimaji, Unyevu
 nyevu. Kwa ujumla maana yake ni kusema kuwa Majini
 hawa wa Sayari ya Mercury wanafanana na maumbile ya
 Mercury (Zebaki).

Muonekano wa Majini hawa ni wa kuridhisha, ni
Wachangamfu katika maongezi, wana Umbo la
Kibinadamu, na wanaonekana kama Shujaa aliye na
silaha.

Mwendo wao ni kama wa Mawingu ya rangi ya Fedha.
 Alama yao ni kuwa wanasababisha Vitisho, Hofu na Woga
 kwa mwenye kuwaita.

Umbo lao Maalum ni la Mfalme anaemuendesha Dubu.

Umbo lao lingine ni la Kijana Mzuri wa Kuvutia.

Umbo lao lingine ni la Mwanamke aliyebeba Kijiti cha
 kukunjia Uzi chenye bonge la uzi.

Umbo lao lingine ni la Mbwa.

Umbo lao lingine ni la Dubu Jike.

Umbo lao lingine ni la Kunguru; Kunguru hawa hutumwa
 kwenda kusaidia katika Kazi za Kichawi na Kijini kwa
 Kuchukua Nguo za Ndani za Watu, Soksi, Vijiko, na vitu
 vingine vidogo dogo kama hivyo. Ndio maana katika aina
 nyingi za Ndege, Kunguru mara nyingi ndio huchukua
 vitu vya ajabu ajabu ambavyo ndege wengine hawawezi
 kuvichukua.

Umbo lao lingine ni la Nguo isiyo na mwili yenye
 kubadilika badilika rangi.

Umbo lao lingine ni la Fimbo, Rungu, Bakora au Gongo
 dogo.
hawa ndiyo majini wanaotawala siku ya jumatano



Majini wa jupiter(Mushtara) - Majini wa Alhamisi
Majini wa sayari hii wanakuwa na mwili mwekundu na
 umbo la kati siyo wakubwa wala siyo wadogo, mwendo
 wao na mwondoko wao ni wa kutisha na wa kuogopesha
 lakini na wapole na wanao ongea taratibu.

Wana rangi ya chuma ambayo inawaunganisha wao na
 Sayari ya Mars (Mariikh). Mwendo wao ni ule wa umeme
 ukiambatana na ngurumo za radi.

Alama yao ni ya mizuka ya watu ambao miili yao ni kama
 iliyojeruhiwa na Simba.

Umbo lao maalum ni la Mfalme mwenye Upanga akiwa
 mgongoni mwa Simba akimwendesha.

Umbo lingine ni la Mtu aliyevalia rasmi Nguo za Chuma za
 Kivita.

Umbo lingine ni la Kijakazi aliyevaa Taji lililopambwa kwa
 Maua.

Umbo lingine ni la Ng’ombe Dume.

Umbo lingine ni la Paa dume

Umbo lingine ni la Tausi

Umbo lingine ni la Nguo ya rangi ya bluu isiyokua na
 mwili.

Umbo lingine ni la Upanga.

Umbo lingine ni la Mti wa Mbuyu.
hawa ndiyo majini wanaotawala siku ya alhamisi


Majini wa Sayari ya Venus (Zuhura) - Majini wa Ijumaa
Majini wa Sayari ya Venus wana Umbo la kati na ambalo
 ni zuri kwa kuliangalia ambapo sehemu yao ya juu ni ya
 dhahabu na sehemu yao ya chini katika mwili ni ya rangi
 nyeupe au kijani.

Mwendo wao ni kama wa mwendo wa Nyota inayong’aa.
 Alama yao ni ile inayofanana na Wanawake wanaocheza
 katikati ya Mduara, huku wakimshawishi na 
kumtamanisha Mwanamazingaombwe ajiunge nao.

Umbo lao maalum ni ni la Mfalme aliyebeba Fimbo ya
 Kifalme huku akiwa anamwendesha Ngamia.

Umbo lao lingine ni la Mwanamke aliye Uchi.

Umbo lao lingine ni la Mbuzi Mwanamke.

Umbo lao lingine ni la Ngamia; ambaye h
uwakilisha
 Shetani mbaya aitwae Cazote.

Umbo lao lingine ni la Njiwa.

Umbo lao lingine ni la Nguo isiyokuwa na mwili ya rangi
 Nyeupe au Kijani.

Umbo lao lingine ni la Mmea uitwao “Savine”.
hawa ndiyo majini wanaotawala siku ya ijumaa