Tibazetu Afrika

Blog hii inahusu tiba za asili juu ya magonjwa mbalimbali ya kimwili na kiroho.Habari,burudani na mambo yote yanayoizunguka jamii.

Contact us

+255 657 739713
Whatsapp/call and sms

Email
Tibazetutz@gmail.com

Watembeleaji

Search

Jumamosi, 23 Septemba 2017

Jinsi wachawi wanavyoharibu nguvu za kiume na kuwafunga wanawake wasipate ujauzito


Wachawi wana uwezo wa kuharibu Nguvu za kiume pia kuzuia
wanawake wasipate mimba kwa kutumia uchawi
au madawa,

Je ni kweli?
 na Je inakuwaje?
Ungana nami kwenye makala hii ndefu uweze kuujua ukweli

Habari hii ya kuwa wachawi huwa wanatumia
Uchawi au madawa katika kuharibu Nguvu za
kiume pia kuzuia wanawake wasipate mimba ni ya
kweli na madawa haya yapo ya aina nyingi.
Mfano katika kitabu cha “ The Encyclopedia of
Witchcraft and Demonology” uk 305 kuhusu
Ligature, (Kukosa nguvu za kiume kutokana na
uchawi) sehemu hii inatoa uthibitisho wa namna
gani Wachawi na watu mbalimbali wanavyotumia
uchawi na madawa kuharibu nguvu za kiume na
kuzuia wanawake wasipate mimba miongoni mwa
baadhi ya watu.
Kuhusiana na jinsi ambavyo watu wanaweza
kufanywa wakose nguvu za kiume au wanawake
wasipate mimba kutokana na Uchawi au Madawa,
watafiti mbalimbali wameelezea njia tofauti
tofauti ambazo watu huwa wanatumia.
Mojawapo ya njia hizo na ambayo inafahamika
zaidi ni ile ambayo, mtu au Mchawi huchukua Uzi
na kuutunga Vifundo ambapo mara nyingine huwa
wanaupaka huo uzi aina fulani ya Dawa ili mtu
asiwe na Nguvu za Kiume na wanawake wasipate
mimba.
Vitendo hivi vya watu kuwafanya watu wengine
wakose Nguvu za Mapenzi vimekuwepo hapa
duniani kwa muda mrefu sana hivyo kuwafanya
watu wengi kusumbuka na kupata shida kubwa
hali ambayo ilipelekea watu wengi kufanya tafiti
mbalimbali juu ya suala hili.
Katika utafiti uliofanywa na Vergil uliojulikana
kama Eclogue (Toleo la nane), alielezea ya kuwa
Mtu anayetaka kumfanya mtu akose Nguvu za
Kiume huwa anafunga Vifundo Tisa (9) katika Uzi.
Mtafiti mwingine aliyejulikana kama Guazzo katika
uchunguzi wake uliojulikana kama Compendium
Maleficarum wa mwaka 1608 ameelezea mambo
mengi kuhusiana na namna watu mbalimbali
wanavyowasababisha watu wengine wakose nguvu
za kiume kwa kutumia uchawi na baadhi ya
madawa.
Alielezea njia kuu wanazotumia Wachawi au watu
ili kuwafanya watu wakose uwezo wa kushiriki
Tendo la ndoa. Yeye alisema ya kuwa Wachawi
huwa wanatumia njia nyingi zaidi ya ile ya
Mwanamume kukosa nguvu za kiume, kwani wao
huwa wanaweza kuwafanya watu wagombane tu
na hii inasababisha wasiweze kufanya tendo la
ndoa.
Kwa ujumla alielezea njia wanazotumia wachawi
katika sehemu kuu Saba (7), kama ifuatavyo:-
1. Mmoja wa Wapenzi, aidha Mwanamme au
Mwanamke amchukie sana Mpenzi wake au
wapenzi wote wachukiane na kutokuwa na hamu
ya kufanya Mapenzi na mwenzake.
2. Wakati Wapenzi wanapokuwa wametenganishwa
Kimwili mbali na mwenzake au Mmoja wa Wapenzi
kuwa anaota ndoto anafanya Mapenzi na mtu wa
kuvutia hivyo kutokuwa na hamu na mwenzake.
3. Wakati Nguvu inayohitajika kwenda kwenye
sehemu ya Kiume ya Mwanamme inapokosekana
na hivyo kusababisha Mbegu za kiume
kutokutoka.
4. Wakati mbegu za Kiume zinapokuwa hazina
Nguvu za kurutubisha mayai ya Mwanamke.
Njia hii huwa inatumiwa sana na mtu anayemloga
mwenzake ili asipate watoto.
5. Wakati Uume unapokosa nguvu ya kuwa thabiti
wakati anapotaka kufanya Tendo la ndoa. Hali
ambayo inapelekea yeye kutokuweza kufanya
tendo la ndoa.
6. Wakati Mwanamke anapolishwa aina fulani ya
madawa aidha kichawi au kwa njia ya kawaida bila
ya yeye kujua ili asiwe na uwezo wa kupata
watoto.
7. Wakati sehemu za siri za Mwanamke
zinapokuwa ni ndogo kuliko kawaida ili asiweze
kufanya mapenzi.
Au wakati sehemu za siri za Mwanamme
zinaposinyaa na kukosa nguvu ghafla wakati
akitaka kufanya tendo la ndoa.
Kwa mujibu wa huyu Mtafiti, hizi zote ni dalili ya
kuwa tayari uchawi umeshafanyika na lengo kuu ni
kuwafanya wapenzi wasiweze kufurahia mapenzi
yao au wakose watoto.
Mtafiti aliyejulikana kama Domenic de Soto
alisema ya kuwa huu uchawi wa kuzuia watu
wasiweze kushiriki tendo la ndoa au wanawake
wasipate mimba ni uchawi wa aina yake ya kipee
kwani lengo la hawa Majini waovu wanaowasaidia
Wachawi siyo kupunguza tendo la ndoa.
Kwani wakifanya hivyo ina maana zinaa itapungua,
hivyo wao hupendelea sana kuwafanya wapenzi
waweze kufanya tendo la ndoa ila wasiweze
kupata watoto na pale inapoonekana ya kuwa hali
ni ngumu zaidi, basi wao ndio huamua kumaliza
au kupunguza nguvu za kiume za mwanamme.
Kwa mujibu wa Domenic de Soto njia inayotumika
zaidi na ambayo ni rahisi ya kusababisha watu
wakose uwezo wa kufanya mapenzi ni ile ya
kufunga vifundo vya uzi.
Uchawi huu ukishafanyika bado utaendelea kuwa
na nguvu mpaka hapo yule mtu aliyefunga hivyo
vifundo atakapovifungua au atakapovilegeza hivyo
vifundo alivyovifuma kwenye uzi.
Iwapo aliyefanya uchawi huo atakufa basi huo
uchawi utaendelea kufanya kazi kwa yule mtu
mpaka hapo vile vifundo vya uzi vitakapoonekana
au kufunguliwa.
Njia nyingine inayotumika katika kuwafanya watu
wakose nguvu au hamu ya kufanya mapenzi ni ile
ya kutumia Dawa ambayo huwa inapakwa kwenye
vile vifundo ambavyo huwa vimefungwa kwenye
uzi au kuwekewa yule ambaye wanataka apate
madhara hayo kwenye chakula au kinywaji chake.
Katika tukio moja lililotokea huko Ufaransa katika
sehemu inayojulikana kama Chateau de
Bassompierre kulikuwa na Mwanamume mmoja
aliyekuwa na umri mkubwa alimuoa Msichana
mmoja mrembo sana na ambaye bado alikuwa
mbichi kabisa.
Yule jamaa baada ya kumuoa yule Msichana, bado
aliendelea kuwa na Mpenzi wake wa zamani,
jambo ambalo lilimkasirisha na kumfanya awe na
wivu mkubwa yule mke wake mpya.
Baada ya muda aliamua kumuomba ushauri jirani
yake ambaye alimpa aina fulani ya Mitishamba
ambayo alimwambia aweke kwenye Supu ambayo
atamtengenezea mume wake.
Baada ya yule mume wake kunywa ile Supu
iliyowekwa Dawa na mke wake, wakati anaamka
asubuhi alishangaa kujiona ya kuwa Nguvu za
kiume zimepotea.
Na kwa sababu alikuwa hawezi kumficha Mke wake
hilo jambo kwa muda mrefu ya kuwa hana tena
nguvu za kiume aliamua kumwambia Mke wake
kuhusu yaliyomkuta.
Mke wake baada ya kugundua alichokifanya na
kuona ya kuwa hata yeye tena hataweza tena
kufanya mapenzi na Mume wake, aliamua
kumwambia ukweli kuhusiana na alichomfanyia
ingawa alimwambia ya kuwa alifanya hivyo
kutokana na penzi zito alilokuwa nalo kwa mume
wake na kuwa roho ilikuwa inamuuma kuona ya
kuwa anashirikiana na mwanamke mwingine katika
mapenzi na mume wake.
Baadae yule Mume wake alimuarifu Mkuu wa ule
Mji ambae alimuita yule jirani yake yule
mwanamke na kumlazimisha ampe yule
mwanamme Dawa nyingine tena ya kumaliza
tatizo lake la kutokuwa na nguvu za Kiume.
Baada ya kupewa ile Dawa alipona na Nguvu zake
za Kiume zikarudi.
Watafiti wengi wamefanya utafati kuhusiana na
Madawa ya kuondoa Nguvu za kiume na kutoa
matokeo ya tafiti zao. Baadhi ya hao watafiti ni
pamoja na De Sotto, Bodin, Remy na Guazzo.
Mnamo mwaka 1567, Mwanake mmoja
alimwambia mtafiti aliyejulikana kama Bodin ya
kuwa kuna njia zaidi ya hamsini (50) tofautu
tofauti za kufanya Uchawi wa Kufunga Uzi ili
kumfanya mtu akose nguvu za kiume au za
kufanya mapenzi na kukosa watoto.
Alisema kuwa kila njia ilikuwa inategemea
malengo yake ni nini, kuanzia

• Kumfunga mtu Mkojo.
• Asiweze kufanya Mapenzi.
• Asiweze kupata Mtoto.
• Aachane na Mpenzi wake kwa Ugomvi n.k
Pia alisema ya kuwa hizo Dawa zipo kama unataka
zimuathiri Mmoja wa Wapenzi au wapenzi wote
wawili.
Nguvu ya Dawa inategemea mhusika mwenyewe
anataka ichukue muda gani, mfano siku moja, au
mwezi mmoja, au milele.
Kumfahamu mtu aliyewekewa au aliyefanyiwa
Dawa kwa ajili ya kumzuia asiweze kufanya
Mapenzi au asiweze kuzaa, inategemea na aina ya
Dawa yenyewe.
Lakini kwa wale waliofanyiwa Dawa ya kutokuwa
na uwezo wa kuzaa watoto, wanaweza kujulikana
kirahisi kwa kuwa huwa wana uvimbe mdogo
kwenye miili yao ambapo kila uvimbe unaonyesha
idadi ya watoto ambao wangezaliwa.
Kuna watafiti wengine ambao walisema ya kuwa
kuna baadhi ya wachawi ambao wana uwezo wa
kuficha sehemu za siri za mwanamume ndani ya
tumbo lake na kuwa sehemu inayokuwepo si
halisi ila ni kiini macho. Na mambo haya yalikuwa
yanatokea sana huko Ujerumani na Scotland
mnamo mwaka 1590.
Katika tukio moja huko Scotland mwaka 1590,
wanawake waliofahamika kama Janet Grant na
Janet Clark walishitakiwa kwa kuwachulia sehemu
za kiume baadhi ya wanaume na kuwapa sehemu
za wanaume wengine ambapo zilikuwa ni sehemu
tofauti kabisa na zile za kwao za asili walizozaliwa
nazo.
Na katika matukio mengine kuna watu ambao
walifanyiwa uchawi na walipoamka asubuhi
hawakuziona sehemu zao za siri, zilikuwa
zimeyeyuka!.
Kulikuwa na matukio mengi ya watu mbalimbali
kuwaona waganga ambao walikuwa na uwezo wa
kuwarudishia uwezo wao wa kufanya mapenzi
uliopotea na kuwezeshwa kupata watoto baada ya
kukaa muda mrefu bila ya kuwapata.
Katika tukio moja mtafiti aliyejulikana kama
Grillandus alielezea jinsi mtu mmoja aliyekuwa na
madaraka makubwa sana jinsi alivyoweza kuwa na
uwezo wa kufanya mapenzi na kufanikiwa kupata
watoto ambao walipelekea yeye kuwa na familia
kubwa na hiyo yote ni kutokana na msaada
aliyeupata baada ya kumuona mganga.
Kuna watu wengi tu mashuhuri na maarufu ambao
waliongelea juu ya watu kutokuwa na uwezo wa
kufanya mapenzi na kukosa watoto
kunakosababishwa na uchawi.
Ivo Charles (aliyefariki mwaka 1115) alikuwa ni
mmoja wa wanazuoni wa mwanzo wa kikatoliki
kuongelea kwa kirefu kuhusiana na haya mambo
ya baadhi ya watu kufanyiwa uchawi ambao huwa
unawaharibia uwezo wao wa kufanya mapenzi.
Mwanafalsafa mmoja mashuhuri sana
aliyefahamika kama Thomas Aquinas aliyeishi kati
ya mwaka 1227 hadi 1274. Alikubaliana na suala
la kuwepo kwa matendo ya watu kufanyiwa uchawi
ili kuwaondolea nguvu zao za kufanya mapenzi.
Alisema ya kuwa ingawa kuna watu wengine
ambao wanapinga ya kuwa hakuna uchawi wa
kuwaondolea watu nguvu za mapenzi. Inabidi watu
wajue ya kuwa mambo haya yapo na yanafanyika
sana.
Alisema ya kuwa wale wanaopinga basi ni kwamba
wanapingana na imani ya kikristo kwani Imani ya
kikristo inasema ya kuwa Mungu Yupo na pia
Shetani naye yupo.
Kwamba kazi za Shetani na Wafuasi wake ni
kuwafanyia watu uchawi na kuwasababisha wakose
watoto na kwa kuwakosesha nguvu za kufanya
tendo la ndoa.
Mwanateolojia (Theologian) mmoja mashuhuri wa
Kanisa Katoliki ambaye alikuwa ni Mfransiska
aliyekuwa anajulikana kama Father Candidus
Brognolus Bergomensi katika kitabu chake
alichokitoa mwaka 1651 kilichojulikana kama
Manuale Exorcistarum alitoa sala katika lugha ya
Kifaransa ambayo ilikuwa inakinga dhidi ya Kukosa
Nguvu za kiume ambao usababishwa na nguvu za
Wachawi.
Hiyo yote ni katika kuthibitisha ya kuwa mambo
haya yapo na kuna kila juhudi zinazofanywa na
watu wa aina mbalimbali ili kuweza kuwasaidia
watu waliothirika na tatizo hilo la wachawi au
watu wengine kuwafanyia Dawa ili wasiweze kuwa
na nguvu za kiume na ili wasiweze kupata watoto.

Kwa Tiba na ushauri
Wasiliana nasi
0653 532036 whatsap
0621 393353
0764 995259
Tibazetutz@gmail.com