Tibazetu Afrika

Blog hii inahusu tiba za asili juu ya magonjwa mbalimbali ya kimwili na kiroho.Habari,burudani na mambo yote yanayoizunguka jamii.

Contact us

+255 657 739713
Whatsapp/call and sms

Email
Tibazetutz@gmail.com

Watembeleaji

Search

Jumamosi, 2 Septemba 2017

dawa 7 za kuongeza nguvu za kike wakati wa tendo la ndoa


hii inahusu hamu ya tendo la ndoa kwa wale wanawake wasiopata kabisa hamu na wale wenye hamu ila wanachoka haraka na kuona kero wakati mpenzi wake yeye anahitaji kuendelea kupiga mpira, hiyo ndio tiba nitakayoielekeza na tiba hii hutibu hadi matatizo ya chango la uzazi kwa wanawake na matatizo ya fangasi sehemu za siri

1 chukua mizizi ya tura tura iliyokomaa chemsha vyema na utumie kwa kunywa asubuhi na jioni lita moja na nusu chemsha mpaka ibaki lita moja na uinywe yote kutwa moja kesho utachemsha mizizi mingine mipya.

2 utachukua unga wa mbaazi na unga wa mdalasini utachanganya na asali kisha utakoroga katika nusu glasi ya maziwa tumia kwa kunywa asubuhi na jioni kwa muda wa siku 21 tu

3 tumia supu ya samaki chemsha vizuri samaki na unywe supu yake asubuhi na jioni kwa siku 5 usiitie chumvi labda ndim au limao

4 kaanga au chemsha dagaa na uweke pilipili ya kutosha tumia na ugali na ufanye hivi mara moja kila siku kwa muda wa wiki moja tu uone ajabu

5 tumia dawa iitwayo mdindadinda ( ipo duka la dawa za asili) utaichanganya na dawa iitwayo mlipu wa unga au unga wa mlonge au unga wa mkunazi koroga katika uji kunywa ujazo wa kikombe cha kahawa dawa hizi ni mujarrab sana.

6 chukua ubani dhukra mjafar mlonge unga wa mbegu zake na zaatar vyote hivi viwe unga utavichemsha na kunywa vitakusaidia mno dawa hii utaitumia siku 14 tu

7 chemsha supu ya kuku mzima tumia kwa kunywa siku mbili na utumie kistwi itakutengenezea mno nguvu za tendo na utaridhia kila namna aitakayo mumeo.