Tibazetu Afrika

Blog hii inahusu tiba za asili juu ya magonjwa mbalimbali ya kimwili na kiroho.Habari,burudani na mambo yote yanayoizunguka jamii.

Contact us

+255 657 739713
Whatsapp/call and sms

Email
Tibazetutz@gmail.com

Watembeleaji

Search

Jumanne, 15 Novemba 2016

DAWA HII INA UWEZO WA KUKUFANYA UINGIE SEHEMU BILA KUONEKANA NA MACHO YA KAWAIDA YA WATU!

INAVYOFANYWA
Kwanza kabisa apatikane paka mweusi ambaye hana kasoro yoyote yaani asiwe mlemavu wala kuchanganyikana na rangi nyingine katika manyoya yake mwilini.
kisha zipatikane kunde(hizihizi za kula)takribani punje 10
kinachofuata ni kumchukua paka huyo na mhusika ambaye ndiye anayetaka kuitumia hiyo dawa anapaswa amchinje paka huyo kwa mkono wake kama anavyochinjwa kuku.
Baada ya kuhakikisha paka huyo ameshakata roho anachukuliwa na panachimbwa shimo sehemu iliyoandaliwa vizuri na anazikwa paka huyo hali ya kuwa macho yake yanatazama juu.
Kwenye macho ya yule paka panawekwa udongo kidogo na kisha panapandwa mbegu tano kila jicho au hata zaidi,na panafukiwa vizuri pamoja na kuweka mbolea
sasa hapo kazi anayoifanya mhusika ni kuhakikisha kila siku anamwagilia maji mpaka mimea ianze kuota kutoka kwenye mbegu hizo alizopanda
ataendelea kuutunza kwa kiwango kikubwa kabisa mmea huo ulioota mpaka ukianza kuzaa kunde.
Kunde zile zikishakomaa,anazichuma zote na sasa zile ndiyo hutumika rasmi kwa ajili ya kazi hiyo.
Sasa endapo mtu huyu atataka aende sehemu na watu wa sehemu hiyo wasimuone(yaani anaweza akaja mpaka hapo ulipo akakaa pembeni yako anachungulia jinsi unavyosoma hii mada kwenye smartphone yako lakini wala humuoni wala kuhisi kitu)basi anakaa mbele ya kioo na anachukua punje moja moja anaweka mdomoni kisha anajiangalia kwenye kioo
ikiwa atajiona kwenye kioo basi mbegu hiyo haifai anaweka pembeni anachukua nyingine
ikiwa amachukua nyingine akaweka mdomoni na akaijitazama kwenye kioo hajioni hiyo ndiyo yenyewe anaihifadhi vizuri
katika hizo kunde zote alizochuma anaweza pata punje 5-7 ambazo zitakuwa hazimuonyeshi kwenye kioo.
sasa akitaka kwenda sehemu na asionekane anachukua ile mbegu anaweka mdomoni na kusema maneno fulani ya kikaguru kisha anatoka(hata kama umekaa nje ya mlango wake humuoni akitoka)anaenda alipokusudia na haonekani kweli.
lakini haonekani na macho ya kawaida tu,mara nyingi wanapokutana na mtu mwenye majini makali njiani huweza kutokea shida kwani mtu yule huweza kumuona kwa uwezo wa jini na akamdhalilisha.
Alipomaliza kuniambia hayo nilipigwa na butwaa na uso ambao dhahiri unaonyesha kutokuamini habari ile,naye aliliona hilo hatimaye akaniambia””sasa babu kama huamini ngoja nikuonyeshe kwa vitendo wewe kaa kimya”
wakati huo mke wake(bibi)alikuwa ameshapika ugali na ameuweka pembeni akisubiri mchunga uliopo jikoni uive ili tujumuike kwenye msosi wa mchana.
Alichokifanaya babu akachukua kikopo kweney mkoba wake wa uganga na akatoa humo ndani punje1 ya kunde kisha akatia mdomoni na kusema maneno fulani ghafla sikuweza kumuona na mara hiyohiyo nikamsikia bibi akilalamika ugali alioupika umechukuliwa hauoni!!!
mara ghafla babu alitokea hapohapo akiwa sahani ya ugali mkononi huku akisema””nilikuwa nataka nimuhakikishie mjukuu wangu kuwa haya mambo yanawezekana”!
kisha akamalizia kusema

”LAKINI DAWA HII HAUTAKIWI KUIFANYA MPAKA UWE UMEFANYIWA MILA MAALUM ZA KUTAMBIKIWA NA MIZIMU LAA SIVYO UTAPATA MADHARA MAKUBWA NA KUJUTA.
Tukawa tumeishia hapo na tukaelekea kwenye meza ya chakula.