Tibazetu Afrika

Blog hii inahusu tiba za asili juu ya magonjwa mbalimbali ya kimwili na kiroho.Habari,burudani na mambo yote yanayoizunguka jamii.

Contact us

+255 657 739713
Whatsapp/call and sms

Email
Tibazetutz@gmail.com

Watembeleaji

Search

Jumatano, 12 Aprili 2017

WAFU WANAPOGEUZWA CHAKULA BADALA YA KUZIKWA



kwanza niweke tahadhari ya picha! Baadhi zitakuwa 

zinatisha

q.jpg 
picha ya tai wanakula mfu, hiyo ni Tibet na kwa imani yao hao tai ni malaika kwahiyo kwa kuwalisha mfu wanapata thawabu ....

Inteligensia ya imani ya dini ni dhana ya kushangaza mno, pengine baadhi ya maono na mitazamo yake vinaacha maswali mengi kuliko majibu 
Mila na tamaduni pia vina mchango mkubwa kwenye haya mambo ya kiimani 
Sisi wakati tukiwashangaa wanaochoma moto maiti, nao wanatushangaa kwakuwa kwao kuzika mfu kwa kumfukia ardhini ni kuinajisi ardhi, ni kuitia nuksi mikosi na balaa, kinachokufa kinapaswa kuteketezwa hii ni imani yao 2013-07-03_205318+-+Copy.pnglakini wakati ukishangaa hawa wanaochoma moto maiti kuna hawa ambao wao hawachomi wanasema ni kuharibu chakula ambacho kingewafaa wengine 
Kwa imani yao ni kwamba uliweza kuishi kwakuwa kuna wanyama ulikula nyama yao na ikakuponya na njaa na afya ukapata 
Kwahiyo unapokufa ni zamu ya nyama za mwili wako kutumika kulisha wengine, huzikwi wala huchomwi moto... Huku Afrika kuna kabila wao maiti hujengewa kichanja na kuachwa hapo iwe chakula cha wanyama, lakini kwa wengine huiandaa kabisa kwa kuikatakatajoejet_com_000559-42_tibetan-funeral_mini1.jpg , zaidi kuna tamaduni nyingine maiti hulishwa kwa wanyama kwenye kusanyiko maalumGunsore_leopard_%28Somnapur_village%2C_Seoni_district%29.jpg

Ukishangaa ya Musa bado hujaona ya firauni...... 
Kumbuka umekula nyama ngapi mpaka umri huu? Usipokuwa mbinafsi na mchoyo nawe utakubali mwili wako uwe chakula cha wengine utakapokufa!