Tibazetu Afrika

Blog hii inahusu tiba za asili juu ya magonjwa mbalimbali ya kimwili na kiroho.Habari,burudani na mambo yote yanayoizunguka jamii.

Contact us

+255 657 739713
Whatsapp/call and sms

Email
Tibazetutz@gmail.com

Watembeleaji

Search

Jumamosi, 7 Januari 2017

MCHICHA NI MBOGA TAMU LAKINI PIA NI DAWA



Ni mboga  maarufu miongoni  mwa  Watanzania. Mbali  na  kutumiwa  kama  mboga, mchicha  pia ni  tiba  ya  matatizo  mbalimbali  ya  kiafya.

Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, mchicha  unaweza  kutibu   matatizo  yafuatayo :

Kuumwa mgongo
Kusafisha njia ya mkojo
Kusafisha damu
Unatibu Magonjwa  ya  Figo
Unatibu minyoo
Unatibu Baridi yabisi
Tezi la shingo
Homa
Kuongeza damu
 Unasaidia kupata haja ndogo kwa wingi
Unarutubisha  uwezo  wa  kuona  vizuri.


JINSI YA  KUTUMIA MCHICHA  KAMA DAWA

MATAYARISHO

Chukua mchicha kilo 1  ya  mchicha, chemsha maji lita 2 na nusu. Yakichemka loweka mchicha kwa dakika 15. Tumia kikombe. Ni bora utumie yote kwa siku . Dozi ni siku 5


KAMA  UNATAKA  KUTIBU MGONGO:

 Chukua mchicha ponda. Chua mara 3 kwa siku. Usiku unapasha moto mchicha kisha unufunga mahali panapouma. Lala nao wakati vuguvugu la joto lake lenye maji ndani (dawa) ikiingia ndani fanya hivyo kwa siku 5, ukibadilisha kila siku (fresh)

KUTUMIA  MCHICHA  KAMA  TIBA  YA TEZI LA SHINGO

Chukua mchicha kiasi kidogo, ponda, fungia shingoni pale penye uvimbe wakati unapolala kwa kitambaa, kwa muda wa siku 5.

Mwenyezi Mungu anatibu
Sisi ni sababu