Tibazetu Afrika

Blog hii inahusu tiba za asili juu ya magonjwa mbalimbali ya kimwili na kiroho.Habari,burudani na mambo yote yanayoizunguka jamii.

Contact us

+255 657 739713
Whatsapp/call and sms

Email
Tibazetutz@gmail.com

Watembeleaji

Search

Jumatano, 11 Januari 2017

UTABIRI MFUPI WA MWAKA HUU 2017 MWAKA ULIOANZA JUMAPILI KATIKA KALENDA ZOTE MBILI HIJIRIA NA MILADIA

Kwa mujibu wa kalenda ya Hijiria Mwaka umeanza kwa siku ya Jumapili Na kalenda ya miladia pia Mwaka umeanza kwa siku ya Jumapili

Sayari yake ni JUA
Buruji yake ni SIMBA

Mwaka wowote ukianza na siku ya JUMAPILI basi mwaka huo utakuwa na
Baridi Kali kwa baadhi ya maeneo hasa nchi za kimagharibi

Magonjwa ya macho,Presha yatawakumba watu wengi hasa viongozi wakubwa wa nchi

Vifo vya watoto na matatizo kwa wanawake wajawazito

Kutazuka vita kubwa kati ya Waarabu na Waajemi

Nzige na mfano wake wataonekana katika baadhi ya maeneo duniani lakini hawataleta madhara ya kitu chochote.

Sultani au mtawala wa Waarabu atakufa au atauawa.

Na Mahujaji watakao kwenda Hijja watarudi salama.

Mwisho wa mwaka mazao yatapendeza sana.

Ngano na shayiri zitaharibika lakini pia zitapungua kwa kiasi kikubwa.

Na majaribu na kesi zitajitokeza kwa watu wengi

Ardhi zinazolima mitende kwa wingi zitakuwa na mavuno mazuri ya mitende yao

Nchi za Magharibi mambo yatakuwa mazuri zaidi katika tawala zao na kutakuwa na makubaliano ya kiutawala

Kutakuwa na fitna kubwa katika nchi za Waafrika wakifitinishwa na nchi za kimagharibi

Ni mwaka wa ndoa na Biashara

Mazao ya kupanda kwa mwaka huu ni yale hayaathiriki na joto Kama dengu,Mihogo,mtama, Hata karanga kwa baadhi ya maeneo zitastawi, nk

Na mahindi na zabibu na makomamanga yatastwi katika baadhi ya maeneo.

Na itaonekana katika watu kuwashwa na upele na maziwa Kutoka kwa wanyama kupungua hii ni kwa sababu jua litamulika sana duniani hivo kuleta ukame na joto.

Kutakuwa na vikao vingi vya kiserikali kwa ajili ya usuluhishi ktk mambo ya kiutawala

Majeshi yatawekwa tayari kuingia vitani


Kwa wale wanaohitaji utabiri wao wa mwaka 2017 wawasiliane nami kwa simu zifuatazo
0653 532036 WHATSAPP VIBER NA IMO
0764 995259