Tibazetu Afrika

Blog hii inahusu tiba za asili juu ya magonjwa mbalimbali ya kimwili na kiroho.Habari,burudani na mambo yote yanayoizunguka jamii.

Contact us

+255 657 739713
Whatsapp/call and sms

Email
Tibazetutz@gmail.com

Watembeleaji

Search

Jumatano, 21 Oktoba 2015

FAIDA NA MUONGOZO WA TENDO LA NDOA


Habari zenu wadau
Docter Ally Chambas's photo. katika masomo mbalimbali juu ya afya zetu yanayoendelea humu, leo ningependa niwajuze mambo muhimu kuhusu tendo la ndoa,na hii imetokana na maradhi yanayotokana na suala zima la ufanyaji mapenzi kiholela kukithiri,kwani watu wengi hufanya tendo hili bila kuzingatia mafundisho muhimu ya wanachuoni,hivyo wengi wamekuwa wakijikuta wanapata matatizo yasiyotarajiwa.
Baadhi ya matatizo yanayotupata kwa kufanya mapenzi kiholela
~kupoteza utu wa mtu
~kudharauliwa
~kupata maradhi mbalimbali kama vile kuziba mkojo,kuishiwa nguvu za kiume,kupata uvimbe sehemu za ndani za figo,au kibofu cha mkojo,magonjwa ya zinaa ukiwemo UKIMWI n.k

Baadhi ya faida kubwa za kufanya mapenzi kiusahihi
~Kuongeza mwendo wa damu

Tendo la ndoa husaidia kuongeza kasi


ya mtiririko wa damu kwenye ubongo
na sehemu nyingine ya viungo vya
mwili, 
hii huchangia kuongeza kasi yamapigo ya moyo na kuboresha mfumo
wa upumuaji. 
Msukumo thabiti wa
damu mpya yenye oxygen na homoni,chembe chembe hai zinapopenya

kwenye mishipa ya damu husaidia
katika uunguzaji wa chakula, pia
huondoa kiasi cha uchafu ambao
 ungesababisha mishipa na kushindwa
kufanya kazi na kumfanya
mwanadamu apate maumivu ya mwili.

~Hupunguza mafuta yenye kileo
(cholesterol)
Tendo la ndoa huweka sawa uwiano wa
mafuta yenye kileo (Cholesterol) nzuri
na cholesterol mbaya na wakati huo
hupunguza kwa ujumla kiasi cha
mafuta yenye kileo mwilini.

~kupunguza maumivu
Wakati wa kufanya mapenzi, homoni
iitwayo oxytosin huzalishwa mwilini
ambayo husababisha kuzalishwa kwahomoni iitwayo endorphin ambazo

hupunguza maumivu kama vile kuvimba
sehemu za viungo (arthritis) maumivu
ya shingo (Whiplash) na maumivu ya
kichwa.

~ulinzi wa tezi ya kibofu (mwanaume)
Majimaji yanayozalishwa katika tezi ya
kibofu (prostate) yakizidi husababisha
kuleta matatizo mwilini. Tendo la ndoa
la mpangilio huondoa uzalishaji wa
majimaji hayo yenye madhara.

~kupunguza mfadhaiko wa moyo.
Kujitosheleza na kupumzisha mwili
baada ya tendo la ndoa ni muhimu kwa
kutuliza akili na kurekebisha mzunguko
wa damu mwilini. Watu wenye kushiriki
tendo la ndoa wanatajwa kushinda
mfadhaiko na kupata usingizi mnono
hasa mara baada ya kumaliza kufanya
mapenzi.


~huongeza uzalishaji wa homoni za kiume(testosterone)na za kike
(oestogen). Faida nyingine inayopatikana
ni kuongeza uzalishaji wa homoni za
kiume na za kike likiwemo suala zima la
hamu ya kufanya tendo hilo
ambapo mhusika hutosheka zaidi ya
yule ambaye hana mazoea ya kufanya
mapenzi. Hata hivyo, baadhi ya
madaktari wamegundua kwamba
ongezeko la homoni za kiume/ kike
huweza kuwakinga wanadamu na
magonjwa ya moyo.


~.kupunguza baridi na mafua
Elimu inaonesha kuwa wanaofanya
tendo la ndoa mara moja au mbili kwa
wiki huongeza 30% ya uzalishaji wa
chembe chembe hai za mwili ziitwazo
Immunogloulin A ambazo huwa na kazi
ya kuulinda mwili dhidi ya magonjwa.


Tendo hili limewekwa kwa sababu kuu3
1.kuhifadhi ukoo

 2.kuyatoa maji ambayo kukaa kwake mwilini kwa muda mrefu kwa mtu aliyebalehe humletea madhara makubwa

3.kukidhi hamu ya tendo hilo

mambo3 ya kujizoesha mwanaume
1. jizoeshe kutembea kwa miguu hata kama una usafiri,kwani ukijizoesha usafiri tu,ipo siku moja utashindwa kutembea

2.Haitakiwi kukaa na njaa muda mrefu kwani kufanya hivyo utumbo hujikunja na unaweza pata magonjwa

3.usiache kufanya mapenzi na mke wako,kwani hata kisima kikikaa muda mrefu bila kuchotwa maji basi maji hayo yatavunda.

hivyo kwa mwanaume yeyote ambaye ameoa akikaa kwa muda mrefu bila kufanya mapenzi basi nguvu za kiume hupungua,uume husinyaa na kuna uwezekano wa kuziba kwa mishipa,

wakati mzuri wa kufanya mapenzi
 1.baada ya kushiba na kupumzika ili chakula kipate kuyayuka tumboni

2.wakati una hamu,usfanye kwa kujilazimisha,ni lazima kuchezeana na kutiana hamu kwanza kabla ya kumuingiza mheshimiwa ikulu

3.wakati ambapo kichwa kimetulia,usifanye mapenzi huku mawazo na fikra zako unafikiria matatizo au mambo fulani tofauti

mambo ya kujihadhari kwenye kufanya mapenzi
1.Usifanye mapenzi na mwanamke mzee sana,au mtoto mdogo sana ambaye haingiliwi

2.Usifanye mapenzi na mwanamke anayeumwaumwa sana utapata maradhi ya kupungukiwa na nguvu za kiume

3.usifanye mapenzi na mwanamke mwenye sura mbaya utapata matatizo ya kupungukiwa na nguvu za kiume

4.usimuingilie mwanamke wakati amechukia na ana hasira nyingi

Mitindo mibaya ya kufanya mapenzi[sex styles]
mume kulala chini na mke juu
~wakati mwanaume unatoa mbegu katika hali kama hii zitatoka kwa tabu sana kwani zinakuwa kama zinapanda mlima,hivyo hazitatoka zote zingine zitabaki na hizi huleta madhara makubwa

~mume akilala chini na mke juu,kuna majimaji huwa yanatoka kwenye uchi wa mwanamke yakiingia kwenye dhakari yatakuletea madhara makubwa

~kumwingilia kwenye duburi[kulawiti] hii ni haraamu kabisa haifai katika sheria za dini na hata wataalam wa afya wamethibitisha kuna madhara makubwa

~kumuingilia mwanamke akiwa hedhini hii pia ni haramu na ina madhara makubwa.