Tibazetu Afrika

Blog hii inahusu tiba za asili juu ya magonjwa mbalimbali ya kimwili na kiroho.Habari,burudani na mambo yote yanayoizunguka jamii.

Contact us

+255 657 739713
Whatsapp/call and sms

Email
Tibazetutz@gmail.com

Watembeleaji

Search

Jumamosi, 24 Oktoba 2015

JAMBO LILILOLETA UADUI KATI YA MAJINI NA WATU~1

Mwenyez mungu alipoiumba mbingu na ardhi na kila kitu kiumbe wa mwisho kuumbwa alikuwa ni bin adam,hii ina maana kwamba majini waliumbwa na walikuwa wanaishi duniani hata kabla ya kuumbwa kwetu sisi binadam na kuishi kwenye ardhi hii

Wakati majini hao wanaishi duniani mwenyez mungu aliwapa sheria ya kuwa wasivuke mipaka na kumuasi yeye mola wao aliyewaumba na wamtii kwa kila atakalowaamrisha.

Lakini majini wakaanza kumuhasi mungu na kufanya ufisadi ardhini na hapo sasa ndipo aliyewaumba akalituma jeshi la malaika kuja kuwafukuza majini hao na kuwapokonya mamlaka yote waliyonayo ardhini,na ndiyo maana majini wengi wakawa ni wenye kukimbia ovyo na wengine wakakimbilia milimani,mapangoni,baharini,mitoni,kwenye mapori makubwa,na katika hali hiyo wakawa ni wenye kufanya makazi yao kwenye maeneo kama hayo

Hapo sasa mwenyez mungu akakusudia kumuumba binaadamu na kumleta duniani awe ndiye khalifa  na ndiyo maana tunayaona maneno hayo kwenye kitabu kitukufu mwenyez mungu anaposema ''INNII JAAILUN FIL ARDHW KHALIIFA

Khalifa maana yake ni mtu ambaye anakuja baada ya fulani kutoka au kutolewa na hapa baada ya kufukuzwa majini ndiyo mwenyez mungu amemleta binadamu kuja kuitawala dunia na kuwa kiongozi baada ya majini kutolewa 

Majini hawa ambao walifanikiwa kukimbilia sehemu tofauti hapo ndipo walipoanza kujenga chuki na kiumbe huyu binadamu baada ya kuona kuwa nafasi yao waliyokuwa nayo wamepokonywa na amekabidhiwa binadamu ndipo ulipozuka uadui mkubwa baina ya viumbe hivi viwili.

fuatilia sehemu ya 2