Tibazetu Afrika

Blog hii inahusu tiba za asili juu ya magonjwa mbalimbali ya kimwili na kiroho.Habari,burudani na mambo yote yanayoizunguka jamii.

Contact us

+255 657 739713
Whatsapp/call and sms

Email
Tibazetutz@gmail.com

Watembeleaji

Search

Ijumaa, 23 Oktoba 2015

FAIDA ZA HABBATSAUDA 1



Dawa hii ni katika madawa makubwa sana ambayo yalikuwa yanatumika tangu enzi za mitume rehema na amani ziwe juu yao

leo ntawajuza baadhi ya faida za habbatsauda ya chenga

baadhi ya magonjwa yanayotibiwa na habbatsauda ni


Hutoa minyoo ya aina zote

huponyesha maradhi ya mabaranga

hutibu homa za vipindi

husafisha malendalenda machafu yanayokuwa kooni na kifuani

huzibua mishipa iliyoziba kwa uchafu au ugonjwa wowote

huondoa gesi tumboni

hukausha unyevunyevu ulio kwenye fuko la chakula kwani fuko la chakula kitaalam halitakiwi kupata unyevunyevu

husaga na kuyeyusha vijiwe vilivyopo kwenye mafigo na kibofu cha mkojo

huteremsha hedhi ambazo zimejifunga kabla ya wakati

hufungua njia ya mkojo na mtu akapata mkojo vizuuuri

hukusanya maziwa na kufanya yatoke mengi kwa mwanamke aliyejifungua kisha maziwa yakawa machache

huponyesha mafua yanayosababishwa na baridi

NAMNA YA KUTUMIA HABBATSAUDA KUJITIBU MOJA KATI YA MARADHI HAYO HAPO JUU KAMA UNAYO
Tumia kijiko kimoja cha chai cha unga wa habbat sauda ndani ya glass1 ya maziwa fresh au chai ya moto au maji ya moto

kunywa kutwa mara3....kwa mwezi mmoja mpaka miezi 6 na utaratibu huu husaidia kutibu maradhi mengi mwilini,kwani kama mtu ataamua kutumia habbatsauda kwa kipimo hicho na ndani ya muda huo nilioutaja,mtu huyo anakuwa na uwezo wa kuzalisha askari wengi mwilini mwake ambao watakuwa wakipambana na maradhi mbalimbali...................

pia ni vizuri habbatsauda ifanywe kama chakula na iliwe wakati wowote hasa baada ya kila mlo 1x3 kwa kipimo nilichokitaja,jambo la msingi sana ni kutumia dawa hii kwa muda unaotosheleza

KUJITIBU VIJIWE KATIKA KIBOFU NA FIGO
Kwa ugonjwa huu chukua unga wa habbatsauda vijiko10 vya chakula kisha changanya na vijiko20 vikubwa vya asali,
matumizi
chota kijiko kikubwa cha mchanganyiko huo koroga ndani ya glass ya maji ya moto,kunywa siku mara3 kwa siku 21......

  KUJITIBU MAFUA
mtu mwenye matatizo hayo achukue unga wa habbatsauda autie kwenye kitambaa awe ananusa kila baada ya muda atapona

hii ni mbegu ya habbatsauda ambayo husagwa na kupatikana unga wake au hukamuliwa na kupatikana mafuta ya habbatsauda,mafuta haya yanatibu maradhi mengi pia ntaelezea kwenye mada nyingne